1 Chronicles 1:34-39
Wazao Wa Sara
34 aIbrahimu alikuwa baba wa Isaka.
Wana wa Isaka walikuwa:
Esau na Israeli.
Wana Wa Esau
(Mwanzo 36:1-19)
35 bWana wa Esau walikuwa:
Elifazi, Reueli, Yeushi, Yalamu na Kora.
36 cWana wa Elifazi walikuwa:
Temani, Omari, Sefo, Gatamu na Kenazi;
Elifazi kwa Timna akamzaa Amaleki.
37 dWana wa Reueli walikuwa:
Nahathi, Zera, Shama na Miza.
Watu Wa Seiri Waliokuwa Edomu
(Mwanzo 36:20-30)
38 eWana wa Seiri walikuwa:
Lotani, Shobali, Sibeoni, Ana, Dishoni, Eseri na Dishani.
39 fWana wa Lotani walikuwa wawili:
Hori na Homamu. Lotani alikuwa na dada yake aliyeitwa Timna.
Copyright information for
SwhKC